Latest Updates

UREMBO:KUCHA ...

UREMBO:KUCHA ...
dgfgh gfgfgh gfgfhgh vcgfg

Nyinginezo, Jiachie chagua, Enjoy - Pinterest style

UREMBO:TENGENEZA MWILI WAKO KWA KUNYWA MAJI YA ALO VERA


Kwa ukweli kuna mshindani mpya wa maji yanayorekebisha mwili wako na kuonekana mrembo zaidi. Watu wa urembo ambao walikazania unywaji wa maji ya dafu sasa wana kitu kipya mtaani, kinywaji cha aloe vera.

Aloe vera wataalamu wanasema kwamba ikinyweka katika maji inasaidia sana kuyeyusha chakula, kuondoa sumu zilizomo mwilini na kuondoa kiungulia lakini kubwa zaidi linabortesha muonekano wako.

Wataalamu wanasema pamoja na kuleta lishe katika mwili kuondoa tatizo la maji kwa ajili ya mwili na ngozi pia ina homoni mbili za Auxin na Gibberellins ambazo huleta kinga dhidi ya viungulia na pia kuleta uponyaji.

Kauliu hiyo imetolewa na mwasisi wa Sublime Beauty, Kathy Heshelow, Gibberellins zinaaminika kuchochea ukuaji wa seli mpya kwa kuimarisha fibroblasts amnbazo hutengeneza collagen.

Maji haya husafisha tishu za ngozi ambazo huathirika sana na sukari na pombe.

Mwili unapokuwa msafi na ngozi nayo inakuwa safi na  maji haya yanasaidia sana kuufanya mwili kuwa bora.

Maji ya aloe vera yanapatikana katika maduka makubwa lakini waweza tengeneza kwa namna hii:
chukua aunzi moja ya juisi changanya na aunzi nane za maji kila siku.

ONGEZA UREMBO KWA KUTUMIA CHUMVI

Ogoza urembo wa ngozi kwa kutumia chumvi
PAMOJA na kutumiwa  kama kiungo  katika mapishi mbalimbali. Chumvi ina umuhimu wake katika suala zima la urembo.
Je, unafahamu kuwa chumvi inaweza kutumika kama kipodozi na kukuacha ukiwa na ngozi nyororo na ya kuvutia?
Kumekuwepo na sababu mbalimbali zinazopelekea warembo kupata matatizo ya ngozi. Kitendo hicho huwafanya warembo husika kupoteza nuru ya ngozi zao na pia matumaini ya kuonekana wenye kuvutia na kupendeza.
Matatizo ya chunusi, ukavu katika ngozi, mafuta usoni na hata mlundikano wa ngozi zilizokufa usoni ni miongoni mwa mambo yanayowakera warembo wengi na hatimaye kupelekea kutumia vipodozi visivyo salama kwa ngozi zao.
 Kwa kutambua hilo wataalamu wa urembo wa asili walikuja na njia hii ambayo haina gharama kubwa ukilinganisha na njia zilizozoeleka na warembo wengi.
 Matumizi ya chumvi yamekuwa na matokeo mazuri katika matatizo mbalimbali ya ngozi, ingawaje si wengi wanalolifahamu hili.
Unachotakiwa kuzingatia ni kuhakikisha kuwa chumvi hiyo haingii machoni mara utakapoanza kuitumia.
Mahitaji.
Chumvi ya unga kijiko 1 kikubwaNamna ya kufanya
 Nawa uso wako kwa maji ya kawaida na kisha chukua kitambaa laini na safi. Chovya kwenye chumvi na kisha sugua katika ngozi yako ya uso taratibu.
Baada ya kupaka katika uso mzima, weka chini kitambaa chako na kisha jisugue kwa kutumia mikono yako. Fanya hivyo hadi utakapoona takataka zinatoka. 
Baada ya kufanya hivyo kwa muda wa dakika mbili, osha kwa kutumia maji ya baridi.
Ni muhimu kufanya zoezi hili mara kwa mara kwani bila hivyo krim au losheni yako unayotumia haitafika katika ngozi pindi unapotaka kufanya hiyo.
Unashauriwa kufanya aina hii ya scrub mara moja kwa wiki ili kupata matokeo mazuri.

UNATUNZAJE MIKONO YAKO? FANYA HIVI

Ili kuweka mikono yako kuwa na muonekano mzuri wa asili na kuwa laini unatakiwa kuipa uangalizi wa kutosha ukiwa nyumbani. Mikono imekuwa ikitumika na kazi nyingi za nyumbani hata ofisini na wakati mwingine tumekuwa tukishika vitu ambavyo vinasababisha mikono kuwa migumu na hata iliyobabuka.
Watu wengi wamekuwa wakitengeneza nyuso zao na kusahau kabisa habari za kutunza mikono kitu ambacho si sawa sawa.
Unatakiwa kujifunza vitu gani vinatakiwa ili kuweza kuiweka mikono yako katika hali nzuri ikiwemo aina ya scrub na moisturizer ambayo itafanya mikono yako kuwa katika hali nzuri kila wakati.
Unaweza kutengeneza mikono yako ukiwa nyumbani  au hata saluni lakini kama utafanya mara moja kwa wiki utakuwa na mikono ambayo iinaonekana vizuri.
Ili kutengeneza mikono yako unatakiwa kuwa na nail file (tupa ya kucha), brashi ya mikono, kitu cha kukatia kucha (hata webe unafaa) losheni ya mikono, taulo sabuni na maji wa vuguvugu.
Unatakiwa kuosha mikono na ukate kucha na kisha anza kuzisugua taratibu kwa kutimua tupa.
Kisha weka maji ya vuguvugu kwenye beseni na tumbukiza mikono kaa kwa muda wa dakika tano ili kuwezesha ngozi ya mikono kulainika.
Kisha anza kusugua mikono taratibu unaweza kutumia kitambaa laini ila unachotakiwa kuhakikisha unasafisha hadi sehemu za katikati ya vidole baada ya hapo suuza mikono yako na ufute kwa taulo halafu paka lotion ya mikono. Njia nzuri pia ya kutunza mikono ni kuhakikisha unakula chakula chenye kulainisha mwili na kunywa maji mengi.
Kama unakuwa hujali mwili wako na hunywi maji mengi unaweza kuwa na mikono mikavu.



TUMIA LIMAO HIVI KUONDOA MADOA MEUSI USONI..

KUMEKUWA na sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na ngozi zisizokubalika.Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe na sigara hata matumizi ya cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila kujua madhara yake kumechangia kwa kiasi kikubwa tatizo hilo.
Ngozi kwa kawaida inatakiwa ijitengeneze yenyewe na si kuitengeneza kwa vipodozi kama wengi wanavyodhani. Ulaji wa matunda na mboga za majani kwa wingi kunywa glasi nane za maji kwa siku ni njia nzuri kama unataka kuwa na ngozi nzuri isiyo na madoa wala ukavu ambao haupendezi.
Wengi wanaacha kula mbogamboga na matunda kwa wingi hata kutokunywa maji ya kutosha na badala yake wamekuwa akitegemea kuwa na ngozi nzuri jambo ambalo ni gumu.Mara kadhaa tumeshuhudia watu wanaopaka cream kali wakiwa kama wameungua usoni huku uso na mwili ukionekana kuwa makavu jambo ambalo linaashiria kuwa kupaka cream  si suruhisho la kuwa na ngozi nzuri.
Kuna watu wamekuwa na ngozi za asili na hata unapowauliza baadhi yao hawajawahi kupaka cream hata siku moja na bado wana ngozi nzuri zinazovutia hao wamekuwa wakila kwa ajili ya kuhakikisha wanatengeneza ngozi zao kutoka ndani.
Pia wengi wanaharibu ngozi zao na kuwa na madoa kutokana na kutumia make up kwa muda mrefu  na hata anapogundua kuwa ana tatizo la madoa amekuwa akijaribu kutumia cream nyingine kwa ajili ya kumaliza tatizo hilo jambo ambali linazidisha madhara kwenye ngozi.
Unaweza kutibu ngozi yenye madoa usoni  pia mashavuni kwa kujitibu na juisi ya limao.
Namna ya kufanya
Chukua  limao lioshe na kisha likamue na kuchuja mbegu zake. Weka juisi hiyo kwenye kikombe na kisha tafuta kitambaa laini  kichovye kwenye juisi ya limao na dondoshea juisi ya limao kwenye sehemu zenye tatizo.
Kaa  kama dakika tano kisha usha uso kwa maji safi.Pia unaweza kuchanganya na asali mbichi  na maji ya limao husaidia pia kuondoa madoa usoni.
Limao lina sifa kubwa ya kuzuia harufu pia unaweza kulitumia katika kuondoa harufu kali ya jasho mwilini  na husaidia kuondoa weusi kwenye kwapa, chini ya macho, mapajani pia.
Chukua kipande cha limao  weka sukari kidogo, sugua.Unatakiwa kutumia kwenye kwapa ambalo ni safi, vizuri kutumia njia hii kabla na baada ya kuoga.