Home » Archive for December 2014
UREMBO:TENGENEZA MWILI WAKO KWA KUNYWA MAJI YA ALO VERA
Aloe vera wataalamu wanasema kwamba ikinyweka katika maji inasaidia sana kuyeyusha chakula, kuondoa sumu zilizomo mwilini na kuondoa kiungulia lakini kubwa zaidi linabortesha muonekano wako.
Wataalamu wanasema pamoja na kuleta lishe katika mwili kuondoa tatizo la maji kwa ajili ya mwili na ngozi pia ina homoni mbili za Auxin na Gibberellins ambazo huleta kinga dhidi ya viungulia na pia kuleta uponyaji.
Kauliu hiyo imetolewa na mwasisi wa Sublime Beauty, Kathy Heshelow, Gibberellins zinaaminika kuchochea ukuaji wa seli mpya kwa kuimarisha fibroblasts amnbazo hutengeneza collagen.
Maji haya husafisha tishu za ngozi ambazo huathirika sana na sukari na pombe.
Mwili unapokuwa msafi na ngozi nayo inakuwa safi na maji haya yanasaidia sana kuufanya mwili kuwa bora.
Maji ya aloe vera yanapatikana katika maduka makubwa lakini waweza tengeneza kwa namna hii:
chukua aunzi moja ya juisi changanya na aunzi nane za maji kila siku.
ONGEZA UREMBO KWA KUTUMIA CHUMVI
Ogoza urembo wa ngozi kwa kutumia chumvi |
Posted by writer
at 9:48 AM,
Add Comment
Read more
UNATUNZAJE MIKONO YAKO? FANYA HIVI
Ili kuweka mikono yako kuwa na muonekano mzuri wa asili na
kuwa laini unatakiwa kuipa uangalizi wa kutosha ukiwa nyumbani. Mikono imekuwa
ikitumika na kazi nyingi za nyumbani hata ofisini na wakati mwingine tumekuwa
tukishika vitu ambavyo vinasababisha mikono kuwa migumu na hata iliyobabuka.
Watu wengi wamekuwa wakitengeneza nyuso zao na kusahau kabisa habari za kutunza mikono kitu ambacho si sawa sawa.
Unatakiwa kujifunza vitu gani vinatakiwa ili kuweza kuiweka mikono yako katika hali nzuri ikiwemo aina ya scrub na moisturizer ambayo itafanya mikono yako kuwa katika hali nzuri kila wakati.
Unaweza kutengeneza mikono yako ukiwa nyumbani au hata saluni lakini kama utafanya mara moja kwa wiki utakuwa na mikono ambayo iinaonekana vizuri.
Ili kutengeneza mikono yako unatakiwa kuwa na nail file (tupa ya kucha), brashi ya mikono, kitu cha kukatia kucha (hata webe unafaa) losheni ya mikono, taulo sabuni na maji wa vuguvugu.
Unatakiwa kuosha mikono na ukate kucha na kisha anza kuzisugua taratibu kwa kutimua tupa.
Kisha weka maji ya vuguvugu kwenye beseni na tumbukiza mikono kaa kwa muda wa dakika tano ili kuwezesha ngozi ya mikono kulainika.
Kisha anza kusugua mikono taratibu unaweza kutumia kitambaa laini ila unachotakiwa kuhakikisha unasafisha hadi sehemu za katikati ya vidole baada ya hapo suuza mikono yako na ufute kwa taulo halafu paka lotion ya mikono. Njia nzuri pia ya kutunza mikono ni kuhakikisha unakula chakula chenye kulainisha mwili na kunywa maji mengi.
Kama unakuwa hujali mwili wako na hunywi maji mengi unaweza kuwa na mikono mikavu.
Watu wengi wamekuwa wakitengeneza nyuso zao na kusahau kabisa habari za kutunza mikono kitu ambacho si sawa sawa.
Unatakiwa kujifunza vitu gani vinatakiwa ili kuweza kuiweka mikono yako katika hali nzuri ikiwemo aina ya scrub na moisturizer ambayo itafanya mikono yako kuwa katika hali nzuri kila wakati.
Unaweza kutengeneza mikono yako ukiwa nyumbani au hata saluni lakini kama utafanya mara moja kwa wiki utakuwa na mikono ambayo iinaonekana vizuri.
Ili kutengeneza mikono yako unatakiwa kuwa na nail file (tupa ya kucha), brashi ya mikono, kitu cha kukatia kucha (hata webe unafaa) losheni ya mikono, taulo sabuni na maji wa vuguvugu.
Unatakiwa kuosha mikono na ukate kucha na kisha anza kuzisugua taratibu kwa kutimua tupa.
Kisha weka maji ya vuguvugu kwenye beseni na tumbukiza mikono kaa kwa muda wa dakika tano ili kuwezesha ngozi ya mikono kulainika.
Kisha anza kusugua mikono taratibu unaweza kutumia kitambaa laini ila unachotakiwa kuhakikisha unasafisha hadi sehemu za katikati ya vidole baada ya hapo suuza mikono yako na ufute kwa taulo halafu paka lotion ya mikono. Njia nzuri pia ya kutunza mikono ni kuhakikisha unakula chakula chenye kulainisha mwili na kunywa maji mengi.
Kama unakuwa hujali mwili wako na hunywi maji mengi unaweza kuwa na mikono mikavu.
TUMIA LIMAO HIVI KUONDOA MADOA MEUSI USONI..
KUMEKUWA na sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na
ngozi zisizokubalika.Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe na sigara hata
matumizi ya cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila kujua madhara
yake kumechangia kwa kiasi kikubwa tatizo hilo.
Ngozi kwa kawaida inatakiwa ijitengeneze yenyewe na si
kuitengeneza kwa vipodozi kama wengi wanavyodhani. Ulaji wa matunda na mboga za
majani kwa wingi kunywa glasi nane za maji kwa siku ni njia nzuri kama unataka
kuwa na ngozi nzuri isiyo na madoa wala ukavu ambao haupendezi.
Wengi wanaacha kula mbogamboga na matunda kwa wingi hata
kutokunywa maji ya kutosha na badala yake wamekuwa akitegemea kuwa na ngozi
nzuri jambo ambalo ni gumu.Mara kadhaa tumeshuhudia watu wanaopaka cream kali
wakiwa kama wameungua usoni huku uso na mwili ukionekana kuwa makavu jambo
ambalo linaashiria kuwa kupaka cream si
suruhisho la kuwa na ngozi nzuri.
Kuna watu wamekuwa na ngozi za asili na hata unapowauliza
baadhi yao hawajawahi kupaka cream hata siku moja na bado wana ngozi nzuri
zinazovutia hao wamekuwa wakila kwa ajili ya kuhakikisha wanatengeneza ngozi
zao kutoka ndani.
Pia wengi wanaharibu ngozi zao na kuwa na madoa kutokana na
kutumia make up kwa muda mrefu na hata
anapogundua kuwa ana tatizo la madoa amekuwa akijaribu kutumia cream nyingine
kwa ajili ya kumaliza tatizo hilo jambo ambali linazidisha madhara kwenye
ngozi.
Unaweza kutibu ngozi yenye madoa usoni pia mashavuni kwa kujitibu na juisi ya limao.
Namna ya kufanya
Chukua limao lioshe
na kisha likamue na kuchuja mbegu zake. Weka juisi hiyo kwenye kikombe na kisha
tafuta kitambaa laini kichovye kwenye
juisi ya limao na dondoshea juisi ya limao kwenye sehemu zenye tatizo.
Kaa kama dakika tano
kisha usha uso kwa maji safi.Pia unaweza kuchanganya na asali mbichi na maji ya limao husaidia pia kuondoa madoa
usoni.
Limao lina sifa kubwa ya kuzuia harufu pia unaweza kulitumia
katika kuondoa harufu kali ya jasho mwilini
na husaidia kuondoa weusi kwenye kwapa, chini ya macho, mapajani pia.
Chukua kipande cha limao weka sukari kidogo, sugua.Unatakiwa kutumia
kwenye kwapa ambalo ni safi, vizuri kutumia njia hii kabla na baada ya kuoga.
Posted by writer
at 9:23 AM,
Add Comment
Read more
Subscribe to:
Posts (Atom)