Latest Updates

UREMBO:KUCHA ...

UREMBO:KUCHA ...
dgfgh gfgfgh gfgfhgh vcgfg

Nyinginezo, Jiachie chagua, Enjoy - Pinterest style

UREMBO:TENGENEZA MWILI WAKO KWA KUNYWA MAJI YA ALO VERA


Kwa ukweli kuna mshindani mpya wa maji yanayorekebisha mwili wako na kuonekana mrembo zaidi. Watu wa urembo ambao walikazania unywaji wa maji ya dafu sasa wana kitu kipya mtaani, kinywaji cha aloe vera.

Aloe vera wataalamu wanasema kwamba ikinyweka katika maji inasaidia sana kuyeyusha chakula, kuondoa sumu zilizomo mwilini na kuondoa kiungulia lakini kubwa zaidi linabortesha muonekano wako.

Wataalamu wanasema pamoja na kuleta lishe katika mwili kuondoa tatizo la maji kwa ajili ya mwili na ngozi pia ina homoni mbili za Auxin na Gibberellins ambazo huleta kinga dhidi ya viungulia na pia kuleta uponyaji.

Kauliu hiyo imetolewa na mwasisi wa Sublime Beauty, Kathy Heshelow, Gibberellins zinaaminika kuchochea ukuaji wa seli mpya kwa kuimarisha fibroblasts amnbazo hutengeneza collagen.

Maji haya husafisha tishu za ngozi ambazo huathirika sana na sukari na pombe.

Mwili unapokuwa msafi na ngozi nayo inakuwa safi na  maji haya yanasaidia sana kuufanya mwili kuwa bora.

Maji ya aloe vera yanapatikana katika maduka makubwa lakini waweza tengeneza kwa namna hii:
chukua aunzi moja ya juisi changanya na aunzi nane za maji kila siku.

ONGEZA UREMBO KWA KUTUMIA CHUMVI

Ogoza urembo wa ngozi kwa kutumia chumvi
PAMOJA na kutumiwa  kama kiungo  katika mapishi mbalimbali. Chumvi ina umuhimu wake katika suala zima la urembo.
Je, unafahamu kuwa chumvi inaweza kutumika kama kipodozi na kukuacha ukiwa na ngozi nyororo na ya kuvutia?
Kumekuwepo na sababu mbalimbali zinazopelekea warembo kupata matatizo ya ngozi. Kitendo hicho huwafanya warembo husika kupoteza nuru ya ngozi zao na pia matumaini ya kuonekana wenye kuvutia na kupendeza.
Matatizo ya chunusi, ukavu katika ngozi, mafuta usoni na hata mlundikano wa ngozi zilizokufa usoni ni miongoni mwa mambo yanayowakera warembo wengi na hatimaye kupelekea kutumia vipodozi visivyo salama kwa ngozi zao.
 Kwa kutambua hilo wataalamu wa urembo wa asili walikuja na njia hii ambayo haina gharama kubwa ukilinganisha na njia zilizozoeleka na warembo wengi.
 Matumizi ya chumvi yamekuwa na matokeo mazuri katika matatizo mbalimbali ya ngozi, ingawaje si wengi wanalolifahamu hili.
Unachotakiwa kuzingatia ni kuhakikisha kuwa chumvi hiyo haingii machoni mara utakapoanza kuitumia.
Mahitaji.
Chumvi ya unga kijiko 1 kikubwaNamna ya kufanya
 Nawa uso wako kwa maji ya kawaida na kisha chukua kitambaa laini na safi. Chovya kwenye chumvi na kisha sugua katika ngozi yako ya uso taratibu.
Baada ya kupaka katika uso mzima, weka chini kitambaa chako na kisha jisugue kwa kutumia mikono yako. Fanya hivyo hadi utakapoona takataka zinatoka. 
Baada ya kufanya hivyo kwa muda wa dakika mbili, osha kwa kutumia maji ya baridi.
Ni muhimu kufanya zoezi hili mara kwa mara kwani bila hivyo krim au losheni yako unayotumia haitafika katika ngozi pindi unapotaka kufanya hiyo.
Unashauriwa kufanya aina hii ya scrub mara moja kwa wiki ili kupata matokeo mazuri.

UNATUNZAJE MIKONO YAKO? FANYA HIVI

Ili kuweka mikono yako kuwa na muonekano mzuri wa asili na kuwa laini unatakiwa kuipa uangalizi wa kutosha ukiwa nyumbani. Mikono imekuwa ikitumika na kazi nyingi za nyumbani hata ofisini na wakati mwingine tumekuwa tukishika vitu ambavyo vinasababisha mikono kuwa migumu na hata iliyobabuka.
Watu wengi wamekuwa wakitengeneza nyuso zao na kusahau kabisa habari za kutunza mikono kitu ambacho si sawa sawa.
Unatakiwa kujifunza vitu gani vinatakiwa ili kuweza kuiweka mikono yako katika hali nzuri ikiwemo aina ya scrub na moisturizer ambayo itafanya mikono yako kuwa katika hali nzuri kila wakati.
Unaweza kutengeneza mikono yako ukiwa nyumbani  au hata saluni lakini kama utafanya mara moja kwa wiki utakuwa na mikono ambayo iinaonekana vizuri.
Ili kutengeneza mikono yako unatakiwa kuwa na nail file (tupa ya kucha), brashi ya mikono, kitu cha kukatia kucha (hata webe unafaa) losheni ya mikono, taulo sabuni na maji wa vuguvugu.
Unatakiwa kuosha mikono na ukate kucha na kisha anza kuzisugua taratibu kwa kutimua tupa.
Kisha weka maji ya vuguvugu kwenye beseni na tumbukiza mikono kaa kwa muda wa dakika tano ili kuwezesha ngozi ya mikono kulainika.
Kisha anza kusugua mikono taratibu unaweza kutumia kitambaa laini ila unachotakiwa kuhakikisha unasafisha hadi sehemu za katikati ya vidole baada ya hapo suuza mikono yako na ufute kwa taulo halafu paka lotion ya mikono. Njia nzuri pia ya kutunza mikono ni kuhakikisha unakula chakula chenye kulainisha mwili na kunywa maji mengi.
Kama unakuwa hujali mwili wako na hunywi maji mengi unaweza kuwa na mikono mikavu.



TUMIA LIMAO HIVI KUONDOA MADOA MEUSI USONI..

KUMEKUWA na sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na ngozi zisizokubalika.Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe na sigara hata matumizi ya cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila kujua madhara yake kumechangia kwa kiasi kikubwa tatizo hilo.
Ngozi kwa kawaida inatakiwa ijitengeneze yenyewe na si kuitengeneza kwa vipodozi kama wengi wanavyodhani. Ulaji wa matunda na mboga za majani kwa wingi kunywa glasi nane za maji kwa siku ni njia nzuri kama unataka kuwa na ngozi nzuri isiyo na madoa wala ukavu ambao haupendezi.
Wengi wanaacha kula mbogamboga na matunda kwa wingi hata kutokunywa maji ya kutosha na badala yake wamekuwa akitegemea kuwa na ngozi nzuri jambo ambalo ni gumu.Mara kadhaa tumeshuhudia watu wanaopaka cream kali wakiwa kama wameungua usoni huku uso na mwili ukionekana kuwa makavu jambo ambalo linaashiria kuwa kupaka cream  si suruhisho la kuwa na ngozi nzuri.
Kuna watu wamekuwa na ngozi za asili na hata unapowauliza baadhi yao hawajawahi kupaka cream hata siku moja na bado wana ngozi nzuri zinazovutia hao wamekuwa wakila kwa ajili ya kuhakikisha wanatengeneza ngozi zao kutoka ndani.
Pia wengi wanaharibu ngozi zao na kuwa na madoa kutokana na kutumia make up kwa muda mrefu  na hata anapogundua kuwa ana tatizo la madoa amekuwa akijaribu kutumia cream nyingine kwa ajili ya kumaliza tatizo hilo jambo ambali linazidisha madhara kwenye ngozi.
Unaweza kutibu ngozi yenye madoa usoni  pia mashavuni kwa kujitibu na juisi ya limao.
Namna ya kufanya
Chukua  limao lioshe na kisha likamue na kuchuja mbegu zake. Weka juisi hiyo kwenye kikombe na kisha tafuta kitambaa laini  kichovye kwenye juisi ya limao na dondoshea juisi ya limao kwenye sehemu zenye tatizo.
Kaa  kama dakika tano kisha usha uso kwa maji safi.Pia unaweza kuchanganya na asali mbichi  na maji ya limao husaidia pia kuondoa madoa usoni.
Limao lina sifa kubwa ya kuzuia harufu pia unaweza kulitumia katika kuondoa harufu kali ya jasho mwilini  na husaidia kuondoa weusi kwenye kwapa, chini ya macho, mapajani pia.
Chukua kipande cha limao  weka sukari kidogo, sugua.Unatakiwa kutumia kwenye kwapa ambalo ni safi, vizuri kutumia njia hii kabla na baada ya kuoga.

Jinsi ya kutengeneza uso ukiwa nyumbani

Kuna namna nyingi ya kutengeneza uso iwe nyumbani au saluni. Pia ni vizuri kama kutakuwa na kuelekezana jinsi ya kutengeneza uso ukiwa nyumbani.
Ni Muhimu ukafuata hatua zifuuatazo;
1.Chukua maziwa  ya mgando na utumie kusafisha uso wako.
2.Scrub kwa kutumia mchanganyiko wa mlozi na karoti au mlozi na jani la chai.
3.Fanya toning ya maji ya uvuguvugu yaliyochanganywa na kipande cha limao  na weka kidogo katika taulo la pamba na futa uso wako mahali pote kaoro kwenye tatizo.
4.Tumia ute mweupe wa yai ambao utakuwa umemwagika katika taulo lako na kujisugua tartibu.
5.Jisafishe na maji ya vuguvugu .
6.Fanya toning tena  kama livyokuwa kwa hatua za tatu juu.
7.Ili kuondoa ukavu za ngozi , kata matango na yabandike katika ngozi.
 
 

Maajabu ya asali katika kufanikisha urembo wako


Utashangaa sana kwamba asali ndiyo hasa kitu kitamu ambacho kwa miaka mingi watu wamekuwa wakikifananisha na raha.
Hii inatokana na ukweli kwamba asali inachukua nafasi ya pekee katika dunia ya mwanadamu.
Nafasi hii ya pekee imo katika mambo mengi mpaka mwenye tiba kwa kaaida asali dawa ya kukabiliana na vitu vingi pamoja na vimelea.
Pamoja na kuwa na antiseptic pia ina moisturizer na pia ina antioxidants na inasaidia kukabiliana na uzee.
Uwepo wa kiwango kikubwa cha sukari katika asali kunaipatia uwezo wa dawa na ndiyo maana kwa miaka maelfu imesaidia watu kutibu vidonda.
Mtaalam mmoja wa ngozi mwenye makazi yake mjini New York City ambaye pia ni daktari, Amy Wechsler anasema hali ya kunyunyurika iliyonayo asali na inayonasa inafanya kuwa kinga imara katika kidonda ambacho kinahitaji kisiingiliwe n vimelea na kutoa mazingira ya kuponya, hivyo asali ni bomba kwa tiba.

 Pamoja na tiba asali ni moisturize babu kubwa kwa ajili ya sura na mwili pia.
Asali ni dawa ya asili ambayo ina uwezo wa kukusanya maji  kutoka ndani ya misuli hadi katika sehemu za juu a ngozi na hivyo kusaidia kuondoa mikunjo.

Mimi nakushauri jaribu moisturizing ya asali ambayo itaondoa ukavu wa ngozi yako na hata kuwasha na kutatarika.

Changanya vijiko vya mezani viwili vya asali na vijiko viwili vya mezani vya maziiwa.

Kisha pasha moto mchanganyiko huo, kisha paka mchanganyiko huo katika uso wako na kupumzika kwa dakika kama kumi hivi.

Kisha jioshe kwa maji ya vuguvugu.Kama unataka kitu kama kosmetiki agiza lotion ya asali ili kuweka sawa ngozi yako.

Hkikisha unanunua lotion ambayo imetengenezwa kwa asali isiyochujwa.

Aina zote za asali zinasaidia kuondoa mikunjo ya uzeeni.