UREMBO:TENGENEZA MWILI WAKO KWA KUNYWA MAJI YA ALO VERA
Aloe vera wataalamu wanasema kwamba ikinyweka katika maji inasaidia sana kuyeyusha chakula, kuondoa sumu zilizomo mwilini na kuondoa kiungulia lakini kubwa zaidi linabortesha muonekano wako.
Wataalamu wanasema pamoja na kuleta lishe katika mwili kuondoa tatizo la maji kwa ajili ya mwili na ngozi pia ina homoni mbili za Auxin na Gibberellins ambazo huleta kinga dhidi ya viungulia na pia kuleta uponyaji.
Kauliu hiyo imetolewa na mwasisi wa Sublime Beauty, Kathy Heshelow, Gibberellins zinaaminika kuchochea ukuaji wa seli mpya kwa kuimarisha fibroblasts amnbazo hutengeneza collagen.
Maji haya husafisha tishu za ngozi ambazo huathirika sana na sukari na pombe.
Mwili unapokuwa msafi na ngozi nayo inakuwa safi na maji haya yanasaidia sana kuufanya mwili kuwa bora.
Maji ya aloe vera yanapatikana katika maduka makubwa lakini waweza tengeneza kwa namna hii:
chukua aunzi moja ya juisi changanya na aunzi nane za maji kila siku.
ONGEZA UREMBO KWA KUTUMIA CHUMVI
Ogoza urembo wa ngozi kwa kutumia chumvi |
Posted by writer
at 9:48 AM,
Add Comment
Read more
UNATUNZAJE MIKONO YAKO? FANYA HIVI
Ili kuweka mikono yako kuwa na muonekano mzuri wa asili na
kuwa laini unatakiwa kuipa uangalizi wa kutosha ukiwa nyumbani. Mikono imekuwa
ikitumika na kazi nyingi za nyumbani hata ofisini na wakati mwingine tumekuwa
tukishika vitu ambavyo vinasababisha mikono kuwa migumu na hata iliyobabuka.
Watu wengi wamekuwa wakitengeneza nyuso zao na kusahau kabisa habari za kutunza mikono kitu ambacho si sawa sawa.
Unatakiwa kujifunza vitu gani vinatakiwa ili kuweza kuiweka mikono yako katika hali nzuri ikiwemo aina ya scrub na moisturizer ambayo itafanya mikono yako kuwa katika hali nzuri kila wakati.
Unaweza kutengeneza mikono yako ukiwa nyumbani au hata saluni lakini kama utafanya mara moja kwa wiki utakuwa na mikono ambayo iinaonekana vizuri.
Ili kutengeneza mikono yako unatakiwa kuwa na nail file (tupa ya kucha), brashi ya mikono, kitu cha kukatia kucha (hata webe unafaa) losheni ya mikono, taulo sabuni na maji wa vuguvugu.
Unatakiwa kuosha mikono na ukate kucha na kisha anza kuzisugua taratibu kwa kutimua tupa.
Kisha weka maji ya vuguvugu kwenye beseni na tumbukiza mikono kaa kwa muda wa dakika tano ili kuwezesha ngozi ya mikono kulainika.
Kisha anza kusugua mikono taratibu unaweza kutumia kitambaa laini ila unachotakiwa kuhakikisha unasafisha hadi sehemu za katikati ya vidole baada ya hapo suuza mikono yako na ufute kwa taulo halafu paka lotion ya mikono. Njia nzuri pia ya kutunza mikono ni kuhakikisha unakula chakula chenye kulainisha mwili na kunywa maji mengi.
Kama unakuwa hujali mwili wako na hunywi maji mengi unaweza kuwa na mikono mikavu.
Watu wengi wamekuwa wakitengeneza nyuso zao na kusahau kabisa habari za kutunza mikono kitu ambacho si sawa sawa.
Unatakiwa kujifunza vitu gani vinatakiwa ili kuweza kuiweka mikono yako katika hali nzuri ikiwemo aina ya scrub na moisturizer ambayo itafanya mikono yako kuwa katika hali nzuri kila wakati.
Unaweza kutengeneza mikono yako ukiwa nyumbani au hata saluni lakini kama utafanya mara moja kwa wiki utakuwa na mikono ambayo iinaonekana vizuri.
Ili kutengeneza mikono yako unatakiwa kuwa na nail file (tupa ya kucha), brashi ya mikono, kitu cha kukatia kucha (hata webe unafaa) losheni ya mikono, taulo sabuni na maji wa vuguvugu.
Unatakiwa kuosha mikono na ukate kucha na kisha anza kuzisugua taratibu kwa kutimua tupa.
Kisha weka maji ya vuguvugu kwenye beseni na tumbukiza mikono kaa kwa muda wa dakika tano ili kuwezesha ngozi ya mikono kulainika.
Kisha anza kusugua mikono taratibu unaweza kutumia kitambaa laini ila unachotakiwa kuhakikisha unasafisha hadi sehemu za katikati ya vidole baada ya hapo suuza mikono yako na ufute kwa taulo halafu paka lotion ya mikono. Njia nzuri pia ya kutunza mikono ni kuhakikisha unakula chakula chenye kulainisha mwili na kunywa maji mengi.
Kama unakuwa hujali mwili wako na hunywi maji mengi unaweza kuwa na mikono mikavu.
TUMIA LIMAO HIVI KUONDOA MADOA MEUSI USONI..
KUMEKUWA na sababu mbalimbali zinazofanya watu kutokuwa na
ngozi zisizokubalika.Mbali na hali ya hewa pia matumizi ya pombe na sigara hata
matumizi ya cream kali ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila kujua madhara
yake kumechangia kwa kiasi kikubwa tatizo hilo.
Ngozi kwa kawaida inatakiwa ijitengeneze yenyewe na si
kuitengeneza kwa vipodozi kama wengi wanavyodhani. Ulaji wa matunda na mboga za
majani kwa wingi kunywa glasi nane za maji kwa siku ni njia nzuri kama unataka
kuwa na ngozi nzuri isiyo na madoa wala ukavu ambao haupendezi.
Wengi wanaacha kula mbogamboga na matunda kwa wingi hata
kutokunywa maji ya kutosha na badala yake wamekuwa akitegemea kuwa na ngozi
nzuri jambo ambalo ni gumu.Mara kadhaa tumeshuhudia watu wanaopaka cream kali
wakiwa kama wameungua usoni huku uso na mwili ukionekana kuwa makavu jambo
ambalo linaashiria kuwa kupaka cream si
suruhisho la kuwa na ngozi nzuri.
Kuna watu wamekuwa na ngozi za asili na hata unapowauliza
baadhi yao hawajawahi kupaka cream hata siku moja na bado wana ngozi nzuri
zinazovutia hao wamekuwa wakila kwa ajili ya kuhakikisha wanatengeneza ngozi
zao kutoka ndani.
Pia wengi wanaharibu ngozi zao na kuwa na madoa kutokana na
kutumia make up kwa muda mrefu na hata
anapogundua kuwa ana tatizo la madoa amekuwa akijaribu kutumia cream nyingine
kwa ajili ya kumaliza tatizo hilo jambo ambali linazidisha madhara kwenye
ngozi.
Unaweza kutibu ngozi yenye madoa usoni pia mashavuni kwa kujitibu na juisi ya limao.
Namna ya kufanya
Chukua limao lioshe
na kisha likamue na kuchuja mbegu zake. Weka juisi hiyo kwenye kikombe na kisha
tafuta kitambaa laini kichovye kwenye
juisi ya limao na dondoshea juisi ya limao kwenye sehemu zenye tatizo.
Kaa kama dakika tano
kisha usha uso kwa maji safi.Pia unaweza kuchanganya na asali mbichi na maji ya limao husaidia pia kuondoa madoa
usoni.
Limao lina sifa kubwa ya kuzuia harufu pia unaweza kulitumia
katika kuondoa harufu kali ya jasho mwilini
na husaidia kuondoa weusi kwenye kwapa, chini ya macho, mapajani pia.
Chukua kipande cha limao weka sukari kidogo, sugua.Unatakiwa kutumia
kwenye kwapa ambalo ni safi, vizuri kutumia njia hii kabla na baada ya kuoga.
Posted by writer
at 9:23 AM,
Add Comment
Read more
Jinsi ya kutengeneza uso ukiwa nyumbani
Kuna
namna nyingi ya kutengeneza uso iwe nyumbani au saluni. Pia ni vizuri
kama kutakuwa na kuelekezana jinsi ya kutengeneza uso ukiwa nyumbani.
Ni Muhimu ukafuata hatua zifuuatazo;
1.Chukua maziwa
ya mgando na utumie kusafisha uso wako.
2.Scrub kwa kutumia mchanganyiko wa mlozi na karoti
au mlozi na jani la chai.
3.Fanya toning ya maji ya uvuguvugu yaliyochanganywa
na kipande cha limao na weka kidogo
katika taulo la pamba na futa uso wako mahali pote kaoro kwenye tatizo.
4.Tumia ute mweupe wa yai ambao utakuwa umemwagika
katika taulo lako na kujisugua tartibu.
5.Jisafishe na maji ya vuguvugu .
6.Fanya toning tena
kama livyokuwa kwa hatua za tatu juu.
7.Ili kuondoa ukavu za ngozi , kata matango na
yabandike katika ngozi.
Maajabu ya asali katika kufanikisha urembo wako
Hii inatokana na ukweli kwamba asali inachukua nafasi ya pekee katika dunia ya mwanadamu.
Nafasi hii ya pekee imo katika mambo mengi mpaka mwenye tiba kwa kaaida asali dawa ya kukabiliana na vitu vingi pamoja na vimelea.
Pamoja na kuwa na antiseptic pia ina moisturizer na pia ina antioxidants na inasaidia kukabiliana na uzee.
Uwepo wa kiwango kikubwa cha sukari katika asali kunaipatia uwezo wa dawa na ndiyo maana kwa miaka maelfu imesaidia watu kutibu vidonda.
Mtaalam mmoja wa ngozi mwenye makazi yake mjini New York City ambaye pia ni daktari, Amy Wechsler anasema hali ya kunyunyurika iliyonayo asali na inayonasa inafanya kuwa kinga imara katika kidonda ambacho kinahitaji kisiingiliwe n vimelea na kutoa mazingira ya kuponya, hivyo asali ni bomba kwa tiba.
Pamoja na
tiba asali ni moisturize babu kubwa kwa ajili ya sura na mwili pia.
Asali ni dawa ya asili ambayo ina uwezo wa kukusanya
maji kutoka ndani ya misuli hadi katika
sehemu za juu a ngozi na hivyo kusaidia kuondoa mikunjo.
Mimi nakushauri jaribu moisturizing ya asali ambayo
itaondoa ukavu wa ngozi yako na hata kuwasha na kutatarika.
Changanya vijiko vya mezani viwili vya asali na
vijiko viwili vya mezani vya maziiwa.
Kisha pasha moto mchanganyiko huo, kisha paka
mchanganyiko huo katika uso wako na kupumzika kwa dakika kama kumi hivi.
Kisha jioshe kwa maji ya vuguvugu.Kama unataka kitu
kama kosmetiki agiza lotion ya asali ili kuweka sawa ngozi yako.
Hkikisha unanunua lotion ambayo imetengenezwa kwa
asali isiyochujwa.
Aina zote za asali zinasaidia kuondoa mikunjo ya
uzeeni.
Posted by writer
at 12:30 AM,
Add Comment
Read more
Subscribe to:
Posts (Atom)